AMKA Be AWARE Be ALIVE

AMKA Be AWARE Be ALIVE Kila mtu ni wa thamani, na kila thamani ya mtu huonekana pale anapogundua kusudi lake la kwa nini amezaliwa na kuanza kulifanyia kazi kusudi hilo.

22/02/2022
Privileged to capacitate; PROFESSIONALISM AND CUSTOMER CARE FOR PETROL ATTENDANTSParticipants: BAKHRESA UNITED PETROLEUM...
03/07/2021

Privileged to capacitate; PROFESSIONALISM AND CUSTOMER CARE FOR PETROL ATTENDANTS
Participants: BAKHRESA UNITED PETROLEUM PETROL ATTENDANTS & DEPOT OFFICIALS

NAO MAKUTANO WAKAMJIBU1. Tumejifunza kuwa hata sisi tuna nafasi ya kufanya makosa na kuhitaji wenzetu watuelewe badala y...
02/07/2021

NAO MAKUTANO WAKAMJIBU
1. Tumejifunza kuwa hata sisi tuna nafasi ya kufanya makosa na kuhitaji wenzetu watuelewe badala ya kutuhukumu.
2. Tumejifunza kuwa ni bora tukahesabu na kuthamini mazuri ya wenzetu na kuwasifia kwa mazuri hayo ili kuwapa motisha ya kuwa busy kuyafanya hayo mazuri hata wakakosa muda wa kuyatenda mabaya tusiyoyapenda.
3. Tumejifunza kutunza funguo/password za furaha na amani ya mioyo yetu sisi wenyewe,badala ya kuwapa watu nguvu ya kutuamulia leo tufurahi au tunune,muda huu tuwe na amani au hasira.
BASI NA ABARIKIWE ASIKIAYE MANENO HAYA NA KUYATENDA.
Amka Upone Be Aware Be Alive

https://youtu.be/hu71slbjIoU
29/06/2021

https://youtu.be/hu71slbjIoU

Marumaru Hotel junior staff receiving continuous professional development training on emotional intelligence and dynamic customer care services on 23rd June ...

Your certificate will get you a job but your attitude will keep your job.Taking Maru Maru hotel team to the highest peak...
18/06/2021

Your certificate will get you a job but your attitude will keep your job.
Taking Maru Maru hotel team to the highest peak of their dreams. Karibu Zanzibar, karibu Celebrations At Marumaruhotel karibu Hemantha Welaratne we are ready to treat you with unforgettable experience.

Unapomwambia mtu ajitahidi awe k**a fulani,je wamjua vizuri huyo fulani? Je wayajua yote yanayomuhusu ambayo yapo sirini...
29/04/2021

Unapomwambia mtu ajitahidi awe k**a fulani,je wamjua vizuri huyo fulani? Je wayajua yote yanayomuhusu ambayo yapo sirini na hajawahi kuyaweka hadharani? Jitahidi uwe k**a Baraka Frances,ivi wewe huyu Baraka unayetaka niwe k**a yeye unamfahamu kiundani kweli? Au unazuzuka tu na unachokiona mtandaoni? Ivi unajua kwa nini yupo ivyo alivyo? Je,upo tayari kukinywea kikombe alichokinywea yeye? Je, ni uzuri wa sura yake au uzuri wa kamera anayotumia? ASIJE HUYU MTU UNAYEMSISITIZA awe k**a fulani akawa kweli k**a huyo fulani kisha ukashindwa kustahimili huo ufulani uliokuwa ukiusisitiza pasipo kuujua undani wake.
1. Mkubali mtu jinsi alivyo,pasipo kumfananisha na fulani. Chungwa na embe yote ni matunda na yote yana umuhimu mwilini mwako. Tafuta thamani ya mtu,usitafute udhaifu wake.
2. Kuwa wewe hivyo unavyotaka mwenzako awe. K**a hawezi jifunza toka kwako hataweza kujifunza toka kwa fulani.
3. Jikubali ulivyo pasipo jilinganisha na fulani. Kuna zaidi ya ukionacho.
4. K**a aliyekuumba alikuumba kwa mfano wake, ya nini kujitaabisha ufanane na mwingine tena? Respect that, remain original and true to yourself.
Amka Awareness Clinic
Baraka Frances - watsapp +255715439205
JE, NA SISI WABADILISHA WATU TABIA TUFANYEJE BAADA YA KUYASIKIA HAYA?
1. Msiwabebeshe watu mizigo ambayo ninyi wenyewe hamuwezi kuibeba mkivaa viatu vyao. Watu huona nuru wakaifuata na sio nuru huona watu ikawalazimisha waifuate.
2. Wekezeni katika upendo,kwani upendo huushinda wingi wa dhambi. Na upendo ni pamoja na matendo sio kauli pekee.
3. Kila unayemuona anafanya usichokipenda ana sababu nyuma yake.
K**a unamwambia mtu aache kudokoa chakula wakati haumpi icho chakula, basi jua ataacha ukiwepo na atadokoa ukiondoka,na usipoondoka atadokoa kwa majirani, kwa kuwa kauli yako haijaondoa NJAA tumboni mwake. (Watu watatafuta mbinu za kuikwepa sheria,na sio kukwepa kutenda makosa ikiwa sababu ya kutenda hayo makosa haijaondolewa)
4. Siku mkijifunza kuacha kuwahukumu watu na kuanza kujifunza kuwaelewa watu mtafunguliwa macho toka katika upofu huu mkuu zaidi ya ule wa Bartholomayo.
Ramadan Kareem

JIFUNDISHE KUNYAMAZA.1. Ukinyamaza utaepuka matatizo yasiyo ya lazima( MITHALI 21:23).2. Kunyamaza wakati fulani maishan...
18/04/2021

JIFUNDISHE KUNYAMAZA.
1. Ukinyamaza utaepuka matatizo yasiyo ya lazima( MITHALI 21:23).

2. Kunyamaza wakati fulani maishani mwako siyo kipawa bali ni nidhamu. ( 1Thesalonike 4:11)

3. Nyamaza unapohisi hasira (mithali 14:17).

4. Nyamaza unapokuwa huna taarifa ya kutosha au ukweli kuhusu unachotaka kusema. (Mithali 18:13).

5. Nyamaza ukijua maneno utakayoyasema yatamkwaza mtu mwenye imani ndogo ( 1Korintho 8:10-11)

6. Nyamaza inapokuwa ni wakati wa wewe kusikiliza na kujifunza ( Mithali 13:1)

7. Nyamaza ukigundua maneno yako yataleta picha mbaya ( Mithali 17:27)

8. Nyamaza ukijua kile unachotaka kusema kitaharibu jina na sifa ya mwenzio ( Mithali 16:27)

9. Nyamaza ukigundua utaaibika baadaye kwa sababu ya ulichokisema ( Mithali 8:8)

10. Nyamaza kwa kufuata mfano wa Yesu kristo (1 Petro 2:21-23)

11. Nyamaza ikiwa wakati ulio nao ni wakati wa kazi ( Mithali 14:23)

12. Mungu akupe neema ya kujenga nidhamu ya kunyamaza maana maneno ya kinywa chako ni mtego.( Mithali 6:2).
Siku njema yenye baraka🙏

Address

Zanzibar City
255

Telephone

+255715439205

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when AMKA Be AWARE Be ALIVE posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to AMKA Be AWARE Be ALIVE:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

AMKA Be AWARE Be ALIVE

Mafanikio halisi katika maisha ya binadamu ni ile hali ambayo anajihisi baada ya kutimiza lengo lolote maishani alilojiwekea, liwe ni lengo kubwa au dogo, liwe limetimia ndani ya masaa kadhaa au ndani ya miaka kadhaa. Na hali hii sio nyingine zaidi ya upendo, furaha na amani. UPENDO, FURAHA, AMANI ni asili ya kila aitwaye binadamu, na endapo chochote kitaingia ndani ya binadamu kilicho kinyume na UPENDO,FURAHA,AMANI basi mwili kupitia ufahamu,hisia,nafsi na viungo vya mwili utahamaki kwa lengo la kujihami na hatimaye kuacha madhara ya mateso,maradhi na vifungo mbalimbali katika maisha ya binadamu huyo. Njia pekee ya kulinda UPENDO,FURAHA,AMANI ni kujitambua na kuanza kuishi kiuhalisia badala ya dhahania kwa kupitia upya elimu,imani,tamaduni,mila na desturi zake alizokusanya tangu utoto na kuondoa kila lenye ukakasi,shaka na viashiria vyenye kutishia uhai wa UPENDO,FURAHA,AMANI ndani ya binadamu.